Browse results

You are looking at 1 - 2 of 2 items for :

  • Primary Language: swa x
  • Search level: All x
Clear All

Ikisiri

Makala hii inalenga kufafanua dhima za kipragmatiki zinazodokezwa kwa kiunganishi ‘na’ baina ya vishazi ambatani katika lugha ya Kiswahili. Dhima hizo huonyesha mahusiano yaliyopo baina ya vishazi vilivyoambatanishwa kwa kiunganishi hicho. Makala hii inaongozwa na nadharia ya Uhusiano ya Sperber na Wilson ambayo inahusu utambuzi wa binadamu na mawasiliano. Data zilizotumika katika makala hii zimepatikana katika machapisho ya kifasihi, hotuba na magazeti. Makala imeonyesha kuwa kiunganishi ‘na’ kina dhima mbalimbali za kipragmatiki ambazo ni uongezi, usababishi, ukinzani, usambamba na ufafanuzi. Dhima hizo ni fasiri ya mahusiano yaliyopo baina ya vishazi ambatani ambayo hayakusemwa kwa uwazi. Makala imeonyesha kuwa kiunganishi ‘na’ ni kiashiria muhimu cha kiisimu kinachomwongoza mshiriki wa mazungumzo kupata fasiri iliyokusudiwa kwa kudhibiti mchakato wa ufahamu. Pia, makala imeonyesha kwamba kiunganishi ‘na’ hutumika sambamba na viashiria vingine vya kiisimu na vya kiulimwengu kuashiria fasiri mahususi iliyokusudiwa baina ya vishazi vilivyoambatanishwa.

In: Utafiti
Author:

Ikisiri

Kisa kinachoelezwa katika simulizi ya Edipode katika tamthilia ya Mfalme Edipode (Sofokile, 1971) kinafanana kwa karibu sana na kisa kinachosimuliwa katika Utenzi wa Nyakiiru Kibi (Mulokozi, 1998). Sababu kubwa zilizochangia kufanana kwa simulizi hizi mbili zinaweza kuelezwa kwa kuzingatia misingi ya kinadharia, hususan Nadharia ya Mageuko na Nadharia ya Msambao. Wakati Nadharia ya Mageuko ikidai kuwa simulizi yoyote ile ni matokeo ya mabadiliko ya ndani ya jamii yanayochagizwa na mazingira, Nadharia ya Msambao inasisitiza kuwa simulizi huenea kutoka sehemu moja hadi nyingine; kamwe haiwezekani simulizi mbili zinazofanana kuibuka katika jamii mbili ambazo hazijawahi kukutana. Makala hii imechunguza sababu za kufanana kwa visa katika simulizi teule kwa kutumia misingi ya nadharia hizo mbili. Kwa kuzingatia hoja mbalimbali, imehitimishwa kuwa simulizi ya Nyakiiru Kibi, pamoja na kutungwa takribani karne 24 baada ya ile ya Edipode, si kiatani cha Edipode. Simulizi hii imechimbuka katika eneo la Maziwa Makuu na inaonekana ni tukio linalofungamana na historia ya jamii husika huku ikijumuisha visakale hapa na pale.

In: Utafiti