Search Results

You are looking at 1 - 1 of 1 items for

  • Author or Editor: Jovitha Lazaro Mayega x
  • Search level: All x
Clear All

Ikisiri

Makala hii inachambua baadhi ya maandiko muhimu yatokanayo na mtaala kwa kutoa ufafanuzi wa kina juu ya dhana na vipengele mahususi vya maandiko hayo ambavyo mwalimu wa somo la Kiswahili hupaswa kuvizingatia katika uwasilishaji wa somo lake. Lengo la uchambuzi huu ni kuonesha athari za kutotumia vizuri maandiko hayo na umuhimu wake kwa walimu katika kufundishia somo la Kiswahili. Ufafanuzi umejumuisha maandiko ya aina tatu nayo ni muhtasari, azimio la kazi na andalio la somo. Uchambuzi huu unatokana na kuwepo kwa matumizi ya maandiko hayo isiyosahihi, walimu kutokutumia maandiko hayo kwa kigezo cha uhaba wa upatikanaji na ukosekanaji wa ufahamu wa matumizi ya maandiko hayo. Kutokana na sababu hizo na kwa kuwa lugha ya Kiswahili kimawanda asili ya matumizi yake ni Tanzania, ni muhimu kuwepo kwa andiko hili ili kumwezesha mwalimu wa somo la Kiswahili kutumia maandiko hayo kwa ufanisi na kuhimiza uandaaji wa maandiko hayo kwa idadi inayotosheleza ili kupunguza uhaba. Data za kuwezesha uandishi wa makala hii zimepatikana kwa njia ya mapitio ya maandiko na matini mbalimbali na kutafsiri rejea zilizoandikwa kwa lugha za kigeni hasa Kiingereza. Imebainika kupitia makala hii kuwa kuna athari zinazotokana na kutotumia maandiko hayo kwa walimu jambo ambalo limesababisha maandiko haya kutotumika ipasavyo.

In: Utafiti